
Msanii wa Singeli Mudy Platnumz anaendelea kupanua wigo wake wa ukaribu na mastaa wa Tanzania, na safari hii macho yote yanaelekezwa upande wa WCB Wasafi.
Taarifa zilizopo zinaonyesha kuwa hivi karibuni page rasmi za WCB zimeanza kuonyesha kuvutiwa na msanii huyo, baada ya kulike baadhi ya maudhui anayopost kwenye mitandao yake ya kijamii.
Hatua hiyo imeibua mjadala kwa mashabiki, wengi wakiona hii kama dalili nzuri na ishara ya hatua kubwa inayokuja kwa Mudy Platnumz ndani ya tasnia ya muziki.
👉 Endelea kufuatilia IK MZIKI kwa updates zaidi za burudani na muziki.
#MudyPlatnumz #WCB #IKMziki #Singeli #BongoFleva
